Kwa sasa teknolojia hii ya ‘wireless charging’ imeshazoeleka kwa kiasi kikubwa sana, licha ya hivyo simu janja nyingi zinakuja na chaja za aina hii katika vifaa vyake.
Simu nyingi kama zile za iPhone, kwa matoleo ya kuanzia X na kuendelea yanaruhusu kuchaji kwa kutumia njia mbili yaaani njia ya kawaida ile ya nyaya na nyingine ya bila utumizi wa waya (wireless charging).
Vipi kuhusu kuchaji bila kutumia nyanya? Je kunaharibu betri au kifaa kwa ujumla?
Hapa twende haraka haraka kidogo, cha kwanza inabidi ujue kwamba kuchaji betri lolote lile kwa njia yeyote ile lazima ilichoshe betri hilo
Hapa maana yangu ni kwamba unaweza kuwa unachaji betri lako kwa njia za kawaida tuu lakini mwisho wa siku ni lazima betri hilo litaishiwa nguvu tuu kadri muda unavyozidi kwenda. Kama lilikua linaweza kaa na chaji siku nzima basi uwezo huo utapungua.
Sio kwamba kuchaji kwa kutumia teknolojia ya bila waya kuna madhara au shida yoyote la-ha-sha lakini vyanzo mbali mbali vinashuri kuchaji kwa kutumia waya wa moja kwa moja.
Sababu kubwa ikielezwa ni kwamba kunakua hakuna nafasi yeyote iyoachwa wazi tofauti na chaja ya bila waya.
Ukiwa unaongelea chaji ya bila waya ni kwamba nishati inaingia katika kifaa chako kwa njia ya mgusano na hapa kinachohitajika ni kuhakikisha kuwa una vifaa vyote vikiwa OG, kuanzia simu mpaka chaja isiyokuwa na waya ili kupata matokeo mazuri.
Kingine ni kwamba katika aina hizi mbili za kuchaji simu hazina matatizo yoyote katika kifaa kwa sasbabu zote zimetengenezwa hivyo, cha msingi ni kuhakikisha kuwa unatumia vifaa ambavyo ni halisia (OG, sio feki).
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, je unadhani ni kuna madhara yoyote kwa chaja ambazo hazitumia nyaya katika simu?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.