Kumekuwa na ubishani kwa wapenzi wa simu hususani kwenye upande wa kamera kwamba ipi simu yenye kamera bora zaidi ya nyingine zilizomo kwenye simu za Samsung Galaxy S10, iPhone XS na Google Pixel 3.
Kupitia tovuti yako namba moja Tanzania kwa masuala ya Teknolojia kwa lugha ya kiswahili ya teknokona, tutawawekea picha zilizopigwa na kamera zilizo kwenye simu hizo kisha utaamua ni ipi picha iliyo kwenye muonekano mzuri na halisi.
Kumbuka matoleo haya ndio ya mwisho kwa makampuni hayo matatu. Samsung Galaxy S10 imetolewa Februari 2019, iPhone XS Septemba 2018 na Pixel 3 imetolewa Oktoba 2018.
Picha tutakazoweka ni zile zilizopigwa kwa kamera ya nyuma na mbele (Selfie).
Sifa za kamera zilizokuwemo katika simu hizo ni kama zifuatavyo hapo chini.
Galaxy S10
Kamera ya Nyuma: 16 MP
Kamera Mbele : 10 MP
Soma uchambuzi wake hapa -> Uchambuzi Simu ya Samsung Galaxy S10
iPhone XS
Kamera ya Nyuma: 12 MP
Kamera Mbele : 7 MP
Soma uchambuzi wake hapa -> Uchambuzi wa Simu ya iPhone XS
Google Pixel 3
Kamera ya Nyuma: 12.5 MP
Kamera Mbele : 8 MP
Soma uchambuzi wake hapa -> Uchambuzi wa Simu ya Google Pixel 3