Baada ya fununu za kutosha tuu kuhusu iPhone SE 2020 ama kwa lugha nyingine toleo la pili kwa mtangulizi wake Apple wameona inafaa kuizindua simu hiyo ambayo inaendana na teknolojia ambayo ipo kwenye umaarufu wake.
Kwa karibu mwaka mmoja sasa palikuwepo na tetesi kuhusu ujio wa iPhone SE 2020 ambayo kimsingi inafanana sana na iPhone 8 lakini pamoja na hayo pia imeboreshwa kipuri mama, memori. Fuata nami kuweza kufahamu mengi zaidi:
Kioo/Muonekano
Kama nilivyokwisha kusema kwenye maelezo yangu ya utangulizi simu hii inafanana kabisa na iPhone 8 kwa muonekano huku urefu wa kioo chake ukiwa ni inchi 4.7 (750*1334px) ambacho ni LCD.
Kamera/Usalama
Uwezo wa kamera kwenye simu husika ni MP 12 kwa kamera ya nyuma (kuu)+flash, MP 7 kwa ile ya mbele. Apple wameweka teknolojia ya kutumia kidole (touch ID) kama sehemu ya kuifanya rununu hiyo iwe na ulinzi.
Kipuri mama/Betri
Moja ya kitu ambacho kinachangia ufanisi bora wa simu janja ni aina ya kiini cha kifa husika hapa namaanisha “Kipuri mama”; kwenye iPhone SE toleo jipya imewekwa A13 Bionic ikiwa ndio teknolojia ya kisasa kabisa kutoka familia ya vipuri vinavyotengenzwa na Apple. Nguvu ya betri ni 1821mAh sawa na kwenye iPhone 8.
Memori/Mengineyo
Apple wameboresha kipengele cha memori mahususi kabisa kwenye RAM ambapo mtiririko wake ni 64GB 3GB RAM, 128GB 3GB RAM, 256GB 3GB RAM. Bei yake inaanzia $399|zaidi ya Tsh. 917,700, GB 128 ni $449|zaidi ya Tsh. 1,032,700 (ile ya GB 256 ni $549|zaidi ya Tsh. 1,262,700) kwa bei ya ughaibuni, haina sehemu ya kuchomeka spika za masikioni, inakuja ikiwa na iOS 13, ina Gigabit-class LTE ambayo ni kasi zaidi kuliko LTE iliyozoeleka, pia inatumia eSIM, inatumia Bluetooth 5, inaweza kutoingia maji umbali wa kina cha mita moja kwa mpaka dakika thelathini (30).
Simu hiyo inatazamiwa kuingia sokkoni wiki ya mwisho wa mwezi Aprili na wengi wakiitazama kama “Pacha” wake iPhone 8 kutokana na kuwa sifa sawa kwenye vipengele mbalimbali.
Vyanzo: MacRumors, GSMArena