Kwa mujibu wa ripoti iliyochapishwa nchini Taiwan na gazeti la United Daily News kwamba kampuni ya Apple itazindua simu mpya yenye laini mbili kwa soko la nchini Uchina pekee.
Simu hiyo ambayo bado haijajulinana wazi, inatarajiwa kuwa na kioo cha LCD cha ukubwa wa inchi 6.1 ikiambatana na simu nyingine.
Taarifa za tangu mwezi Aprili 2018 zilieleza mpango wa Apple kuja simu yenye laini mbili kwa mara ya kwanza na hili lilipata nguvu zaidi wakati mfumo endeshi wa simu za iPhone wa iOS toleo la 12 lililopotoka na kuonesha lipo jambo la namna hiyo.
Katika uzinduzi wa simu za iPhone kwa mwaka 2018 zinatazamiwa kutoka simu za matoleo matatu; iPhone ya inchi 5.8, 6.5 na 6.1 ambayo itakuwa inatumia kadi mbili za imu.