Ni wazi kuwa teknolojia ya kutumia simu bila ya kwa na laini inayoonekana (eSIM) kwa sasa imkeua sana na kwa sasa teknolojia hii imesambaa sana katika bara ya Asia na Ulaya.
Lakini ukijaribu kufikia kwa umakini sana unaona kabisa teknolojia ya kuchomeka laini katika simu inaenda kupotea kabisa (alafu tunayo kwa muda mrefu sana).
Mpaka sasa kuna baadhi ya matoleo ya iPhone ambayo tayari yanatumia teknolojia hii ya eSIM lakini huku yakiwa yanatumia na laini ya kawaida kwa maana nyingine matoleo hayo yanatumia laini mbili
eSIM ni ile laini ya kimtandao ambayo hauiweki moja kwa moja kama laini za kawaida bali unaunganishwa nayo kwenye mtandao na mtoaji huduma wa mtandao husika mfano tigo, voda n.k
Apple walianza tengeneza iPhone zenye huduma ya eSIM katika matoleo ya iPhone XS na kwa sasa hata katika toleo la iPhone 13 bado teknolojia hii ipo.
Simu janja nyingi ziko katika mchakato wa kuhakikisha kuwa inatoa matundu mengi katika jumba la simu yake. Tumeona simu nyingi zikiondoa tundu la spika za masikio (earphone) na mengine mengi
Pengine kwa Apple tundu linalofuata ni hilo la laini? Au vile vile tusisahau kuwa simu ikiwa inatoa matundu mbali mbali huwa inajipa uwezo wa kuongeza vitu vingine
Kwa mfano betri la simu kutoka iPhone liliongezeka ukubwa baada ya tundu la spika kuondolewa, kwa hiyo vitu kama hivi vipo yaani kinaondolewa kitu ili kukipa nafasi kitu kingine.
Mpaka sasa inasemekana kuwa katika toleo la iPhone 14 kuna baadhi ya simu hizo zitakua na toleo ambalo lina eSIM tuu na toleo hilo litakua linauzwa katika soko maalumu huku matoleo mengine yakiwa ni ya kawaida na kuuzika duniani kote.
Chanzo: GSMArena
Ningependa kusikia kusikia kutoka kwako, je wewe ungependelea kuwa na simu ya aina hii ambayo ina laini ya kimtandao, au unapendelea hizi za kawaida tuu? Niandikie hapo chini kwenye uwanja wa comment.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.