iPhone 12 Pro Max ni moja ya simu zinazotengezwa na Apple ambazo zinategemewa kuzinduliwa baadae mwaka huu na kama ilivyo kawaida upo mtindo wa kupata tetesi mbalimbali kuhusu rununu/bidhaa kabla ya kutoka rasmi.
Ni desturi ya kampuni tajiri namabari moja kwenye masuala ya teknolojia kufanya uzinduzi wa bidhaa zake mbalimbali mwezi Septemba lakini kabla ya kufika huko tayari tovuti mbalimbali zimeshaweza kupata taarifa kadha wa kadha kuhusu simu janja toleo la 12 Pro Max.
Muonekano wa simu hiyo umeweza kutoa mwanga wa iwapo simu hiyo itakuwa na urefu wa wastani au la kama ambavyo tunazifahamu rununu mbalimbali zilizopo sokoni/zimeshazinduliwa. Kiujumla rununu hii inafanana na iPhone 5s ingawa si kwa sifa za kiundani.
Kwa mantiki hiyo simu hiyo inaaminika kuwa kioo chake kitakuwa na urefu wa inchi 6.7, kamera tatu (3) upande wa nyuma huku mojawapo ikiwa na teknolojia ya LiDAR. Ingawa kwa picha ambazo zimevuja zinaonyesha mpangilio wa muonekano ule wa nyuma bado haujakamilika kwa maana ya kwamba bado inaendelea kuboreshwa.
Mpaka sasa inaelezwa kuwa muundo wa simu hiyo umekamilika kwa asilimia 70 vikiwa imebaki vipengele vichache kuikamilisha kadri ambavyo itawapendeza wahusika tayari kwa kuzinduliwa baadae mwaka huu na hatimae kuingia sokoni.
Vyanzo: GSMArena, Forbes
One Comment
Comments are closed.