iOS ni progamu endeshaji ambazo zinapatikana katika vifaa vya iPhone na iPad. Kwa sasa toleo ambalo lipo ni lile la iOS 14 lakini iOS 15 bado iko njiani.
Tunajua kabisa kila toleo lazima linakuwa linakuja na kitu cha utofauti na toleo la nyuma (maboresho) jambo hili ni moja kati ya vitu vinavyowapa watu shauku juu ya toleo lijalo
iOS 15 Itakuwa Inapatikana Katika Vifaa Hivi
- iPhone 7
- iPhone 7 Plus
- iPhone 8
- iPhone 8 Plus
- iPhone X
- iPhone XR
- iPhone Xs
- iPhone Xs Max
- iPhone 11
- iPhone 11 Pro
- iPhone 11 Pro Max
- iPhone SE (2020)
- iPhone 12 mini
- iPhone 12
- iPhone 12 Pro
- iPhone 12 Pro Max
- Matoleo yanayokuja ya iPhone 13 na kuendelea
Japokuwa hakuna taarifa rasmi kuhusiana na sifa ambazo zitakuwa zinapatikana katika iOS 15 inasemekana kwamba kutakua na maboresho makubwa katika eneo la ‘Notification’
Vile Vile katika iPad, inasemekana kwamba itabadilisha uso wa nyumbani (Home Screen) hali ambayo itabadilisha kabisa jinsi watu walivyokuwa wakitumia iPad zao.
Katika iMessage kuna maboresho mengi sana na kwa taarifa zilizopo ni kwamba kampuni imejikita sana katika kuhakikisha inachuana vikali na WhatsApp.
Tazama Video Hii Kwa Ufupi (Muonekano Ambao Unadhaniwa)
Ni wazi kuwa mengi hayako wazi kwani Apple wenyewe bado hawajaanda uzinduzi na kusemea kwa kina juu ya iOS 15. Ni lini sasa tutegemee kwamba iOS hii itaachiwa na sisi kujua vipengele vyote?
Toleo kwa ajili ya ‘developers’ litatoka juni 7-11 katika WWDC, baada ya developers kulitumia kidogo na kulifanyia majaribio ndio litaanza kupatikana katika vifaa vyote vya iPhone (kuanzia iPhone 7).
Katika WWDC, ndio majibu kamili na sifa za iOS 15 zitajulikana kwa udhahiri kabisa kwani kwa sasa ziko fununu tuu
Kuwa nasi mara kwa mara ili kujua mpaka mwisho wa hili
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako, Niandikie Hapo Chini Katika Eneo La Maoni. Pia Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Pendwa Wa TeknoKona Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
No Comment! Be the first one.