Instagram imeendelea na tabia yake ya kuiga vitu kutoka mtandao wa Snapchat, Instagram leo inaleta maboresho katika mtandao wake ambayo pamoja na yote yataleta vitu vitatu ambavyo vyote vipo na vinafanya vizuri katika mtandao wa Snapchat.
Instagram imeendelea na mchezo wa kuuiga Snapchat baada ya kuleta mabadiliko mapya, sasa kama ilivyokuwa kwa Snapchat watu wataweza kuweka filter katika selfie zao ( kama zile za masikio na ulimi wa mbwa katika Snapchat) unaweza kuweka Hashtag katika picha ambayo itakuwa kama stika pia watumiaji wanaweza kufuta michoro ambayo wameichora katika picha kwa kutumia kifutio ama eraser.
Je mtindo huu wa kuiga Snapchat unawasaidia Instagram?! ama ndio unauua mtandao huu?.
Ukweli ni kwamba Instagram imesaidiwa saana na kuiga kutoka kwa Snapchat maana Stories ambayo ni kitu kilichoigwa imefanikiwa kufikia watumiaji milioni miambili ukilinganisha na watumiaji milioni mia moja na sitini ambao walilipotiwa kutumia Snapchat wakati ikijiandikisha katika soko la hisa.
Mabadiliko haya yanategemea kuwafikia lini watumiaji?
Kwamujibu wa mtandao wa Techcrunch mabadiliko haya yanaanza kutolewa leo kwa watumiaji wa ulimwengu mzima na wa OS zote, hivyo siku si nyingi tutaanza kuona mabadiliko haya katika akaunti zetu.
Tuambie unaonaje mabadiliko haya na mtindo huu wa Instagram kuiga vitu kutoka Snapchat, Je watatoboa ama ndio wanajimaliza wenyewe??