Instagram yamfungia ndugu wa aliyekuwa Rais wa Marekani, John F Kennedy kutokana na kusambaza taarifa zisizokuwa sahihi kuhusu maambukizi ya Covid-19.
Bwana Robert F. Kennedy Jr ni mpwa wa aliyekuwa Rais wa Marekani, ambaye ni maarufu pia kutokana na kuuliwa kwa shambulio la risasi. Rais John F Kennedy alikuwa rais wa wa Marekani.
Kwa kipindi kirefu Bwana Robert F. Kennedy Jr ambaye ni mwanasheria na mwanamazingira amekuwa akipost habari ambazo zinatuhumiwa kuwa hazina ukweli wowote juu ya janga hilo. Amekuwa akipinga vikali utumiaji wa chanjo za Covid19 na kuzungumza mengi ambayo serikali na watu wengine wamekuwa kuyapinga wakisema hayana ukweli wowote.
Facebook wamesema wataendelea kuchukua hatua kali dhidi ya akaunti zozote Instagram au Facebook zitakazokuwa zinatuma jumbe ambazo si zahihi kuhusiana na janga la Covid 19.
Suala hili kufungia akaunti kutokana na misimamo yao limeanza kuwa gumzo hasa baada ya Twitter, Facebook, Instagram na wengine kufunga akaunti za aliyekuwa Rais wa Marekani, Bwana Trump. Je suala hili haliingilii suala la uhuru wa maoni? Kama wametenda kosa – kushitakiwa sio ndio njia sahihi kuliko kuondoa akaunti zao? Tuambie maoni yako.
Chanzo: TheVerge na Facebook
No Comment! Be the first one.