App maarufu ya mambo ya picha na video – Instagram yafikisha watumiaji milioni 500, hii ni idadi ya watumiaji milioni 100 zaidi ukilinganisha na mwezi wa 9 mwaka jana.
Mtandao wa kijamii huu unaomilikiwa na Facebook umetoa taarifa rasmi ya idadi ya watumiaji wake masaa machache yaliyopita.
Katika taarifa hiyo pia wameonesha idadi ya watumiaji hai kwa siku kuwa ni watumiaji milioni 300, yaani hii inamaanisha kuna watumiaji milioni 300 wanaofungua app ya Instagram kila siku.
Pia wanajivunia kuona ukuaji wa watumiaji wa app hiyo unakizidi kuongezeka nje ya nchini Marekani, katika taarifa yao wamesema zaidi ya watumiaji asimilia 80 ya app hiyo wapo nje ya nchini Marekani.
Idadi ya watumiaji wa mtandao huu wa kijamii umekua mara mbili ndani ya miaka miwili, kampuni ya Instagram na app yake ilinunuliwa mwaka 2012 na mtandao mkubwa wa kijamii wa Facebook kwa takribani dola bilioni 1 za Kimarekani.
Je wewe ni mtumiaji wa kila siku wa app ya Instagram? Hongera, ni mmoja kati ya watu milioni 500 duniani kote!
Chanzo: Instagram Blog
2 Comments
Comments are closed.