Kipengele cha “Stories” kwemye Instagram kimekuwepo kwa miaka sasa na kimekuwa kikifanyiwa maboresho ambayo huwa yanapokelewa katika mtazamo chanya na hasi.
Facebook ambayo ndio inamiliki Messenger, WhatsApp, Instagram imekuwa ikileta maboresho kwenye programu tumishi ambazo inamiliki. Wataalamu wa uandishi wa programu wapo kazini kuleta maboresho kwenye kipengele cha “Stories” ndani ya Instagram hivyo kukifanya kivutie kwa namna yake.
Swali dgogo tuu; Instagram stories ni nini?
Hiki ni kipengele ambacho kinapatikana kwenye Instagram, Facebook ambacho mtu anaweka chapisho lake (inaweza kuwa picha, picha mnato au ujumbe wa maandishi) na mara baada ya mhusika kupandisha hewani kile ambacho anataka wengine wakione kinakuwa kwenye uso wa mbele juu kabisa hivyo kuonekana kwa urahisi.
Kipengele cha “Stories” kwenye Instagram.
Watumiaji wa Instagram mtakubaliana na mimi kuwa tunaperuzi machapisho ya watu kwenye Instagram Stories lakini hatuna uwezo wa kuonyesha kuwa tumevutia na chapisho fulani, si ndio? Hilo sasa huenda likabadika kwani kuna maboresho yanapikwa ambayo yatamwezesha mtumiaji wa Instagram kuonyesha hisia zakekuhusu chapisho fulani kwenye “Stories“.
Inaaminika kuwa kwenye maboresho hayo mtu atakuwa na uwezo wa kuonyesha kupendezwa na chapisho husika mara nyingi tuu (zaidi ya mara moja). Pia, aliyechapisha hata pokea ujumbe wa kumwambia fulani na fulani wamependa kile alichokiweka kwenye “Stories” lakini itakuwepo sehemu ambayo mhusika ataweza kufahamu kile alichokiweka kimewapendeza wangapi.
Kwa sasa kipengele hiki bado hakijaanza kuonekana/kufanya kazi na pengine kikapatikana kwa wote au la! Hivyo, kitu cha kufanya ni kuendelea kutufuatilia na tutazidi kuwahabarisha yale yanayoendelea.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
No Comment! Be the first one.