Instagram kuwasaidia wenye uraibu (addiction) kwenye matumizi ya app hiyo maarufu. Kampuni ya Meta, mmiliki wa Facebook, Instagram na apps zingine maarufu, imesema inachukua hatua kupunguza utumiaji mbaya wa app hiyo.
Huduma mpya inayokwenda kwa jina la ‘Take a Break’, itaanza kwenye mataifa ya Marekani, Uingereza, Ireland, Kanada, Australia, na New Zealand kabla ya kusambaa katika mataifa mengine yote. Huduma za Facebook na Instagram kwa kipindi kirefu zimekuwa zikilaumiwa kwa kusababisha na kulea matumizi mabovu, hasa hasa yanayohusisha vijana. Kupitia huduma hii Meta wanaonesha kujali afya za watumiaji wake hasa hasa vijana wadogo.
Tayari ili kupunguza uraibu Instagram ilifanya mabadiliko katika masuala kuonesha ‘Likes’ za kwenye picha, baada ya kuonekana vijana wengi wakiangaika na kujaribu kufanya lolote ili waweze kupata Likes nyingi.
Kupitia huduma hii mpya watumiaji wataweza kuweka mpangilio (setting) ya kukumbushwa kupumzika kila baada ya dakika 10, 20 au 30 za utumiaji wa app ya Instagram.
Tuendelee kutegemea kuona mabadiliko mengi kwenye huduma za Facebook na Instagram, kampuni mama ya Meta inapitia changamoto kadhaa na vyombo vya kisheria kuhusu jinsi huduma hizi za kijamii zinavyoathiri vijana.
Vyanzo: Meta, CNN
No Comment! Be the first one.