Mtandao wa Instagram umeongeza idadi ya watumiaji wake hivyo familia inazidi kukuwa kwa kasi ya hali ya juu.
Tangia mwezi wa nne mpaka sasa Instagram imefikisha watumiaji milioni 800 kwa mwezi kutoka watumiaji milioni 700 kwa mwezi
Inamaanisha katika rekodi zake haikuwahi kuongeza idadi ya watumiaji wengi hivyo (milioni 100) ndani ya kipindi cha muda mchache kama sasa. Hivyo basi inaonyesha dhahiri kuwa idadi ya watumiaji inakua kwa kasi kubwa sana
Instagram kumbuka ndio mtandao wa kijamii ambao unasifika sana na umejichukulia umaarufu mkubwa katika maswala mazima ya picha.
Idadi ya watumiaji imezidi kupanda baada ya mtandao huo kukopi baadhi ya vipengele katika mtandao wa kijamii wa Snapchat.
Kwa haraka haraka inawezekana kabisa kwa Snapchat ikashindwa kupambana na Instagram,, Hebu fikiria tuu kuna ulazima gani wa kutumia App mbili ambazo huduma zake zinafanana?
Mpaka sasa Instagram ina watumiaji wengi kuliko Snapchat, Vipengele vipya vingi vya Instagram vimekopiwa Snapchat. Hili pekee linaweza wasababisha wengi kubakia katika mtandao wa Instagram.
La muhimu ni kwamba ni vigumu sana mtu kutumia mitandao miwili ya kijamii ikiwa anapata huduma sawa hivyo basi mkubwa atabaki kuwa mkubwa tuu