Wengi wanapenda kwenda Live katika mtandao wa kijamii wa Instagram. Mtandao huo umekua ni moja ya sehemu maarufu ya kurusha matokeo ya moja kwa moja kwa nddugu, jamaa na marafiki.
Kwa sasa Mtandao huo uko katika majaribio ya kuangalia kama zoezi hilo litafanikiwa huku screen ikiwa inagawanyika.
Yaani hapa iko hivi wakati mtu anawekwenda Live katika mtandao huo ana uwezo wa kumualika mtu mwingine nae akaenda Live.. Kitakachofanyika ni kwamba ‘Screen’ itagawanyika mara mbili na kisha zitaonekana video mbili (Live).
Mtazamaji atakuwa na uwezo wa kuziona video zote hizo mbili na pia atakuwa na uwezo wa ku’comment katika video hizo kama kawaida.
Mpaka sasa haijulikani siku kamili ambapo kipengele hichi kitaachiwa rasmi, kwani kwa sasa kampuni imechagua watu wachache tuu kukifanyia majaribio.
Kampuni imesema dunia nzima itegemee kipengele hichi katika miezi ya usoni.
Kampuni kwa sasa inafanya vizuri sana kwani inaufanya mtandao usionekane kama ni wa ku’share picha tuu, bali unaonekana una mambo mengi kama vile storie, LiveStream na mambo mengine mengi.
Mtandao unazidi kupiga hatua kila siku na kama kipengele hiki kikitoka duniani kote basi itakua ni msaada mkubwa sana kwa watu. Hebu fikiria msanii mmoja anaweza akaenda Live na msanii mwenzake katika ukurasa mmoja.