Mtandao wa kijamii wa Instagram umekuwa ukifanya maboresho ya huduma zake kupitia taarifa wanazopata kwenye tafiti mbalimbali wanazaofanya kuhusiana na matumizi ya jukwaa hilo. Hivi karibuni Mkuu wa Instagram Adam Mosseri ametangaza kuwa kampuni hiyo imeanza kujaribu kipengele kipya wiki hii kiitwacho “Pumzika”.
Kitufe hicho ambacho kitaongezewa kitawawezesha watumiaji kupumzika kutumia programu ya Instagram. Kitufe hichi kitakuwa ni cha hiari kila mtu anauwezo wa kukitumia endapo ataamua na kitakuwa kinakukumbusha kila baada ya dakika 10, 20 au 30 kuwa upumzike kutumia programu ya Instagram.
Uongozi wa Instagram ulisema pia kuwa kipengee hicho kipya hakitaadhiri ufanyaji kazi wa programu yao. Vikumbusho vipya vya “Pumzika” vinazinduliwa wiki hii kama jaribio na idadi ndogo ya watumiaji, kwa sasa, lakini kampuni inatarajia kusambaza kipengele hicho hadharani katika miezi ijayo.
Chanzo: Techcrunch
No Comment! Be the first one.