Instagram Direct imekuwa ikiambatanishwa kwenye app ya Instagram lakini pia kumekuwa na mjaribio ya kuigeuza kuwa app ya kujitegemea. Tayari Facebook waliingiza app ya kujitegemea kwenye takribani nchi 6.
Facebook wamekuwa ni watu wa kutoa masasisho kila mara na yamekuwa yakijumuisha maboresho makubwa kwa madogo. Kwa muda mrefu wamekuwa wakifanya majaribio ya kuwa na app inayojitegemea ikienda kwa jina la Instagram Direct na ikiwe imelenga kuwa mshindani wa moja kwa moja wa Snapchat.
Katika taarifa za hivi karibuni zinaonesha kuwa Facebook wanaachana na mpango huo.
Je, Instagram Direct ni nini?
Hiki ni ile alama ya tiara au jumlisha (+) inayoonekana upande wa klia juu baada ya kuingia kwenye Instagram. Kazi yake ni kuwezesha kutuma na kupokea ujumbe mfupi wa maandishi katika faragha au kama vijana wanavyosema “Nifuate DM” 😆 😆 .
Je, hatua hiyo ina maana haitawezekana tena kutuma/kupokea jumbe kwenye Instagram?
La hasha! Watumiaji wa Instagram wataendelea kutuma na kupokea jumbe kama kawaida. Facebook itakuwa imeona katika masoko waliofanyia majaribio huduma hiyo kujitegemea haijapokelewa vizuri na hivyo wameamua kuachana na mpango huo.
Vyanzo: Phone Arena, TechCrunch
{Makala hii ilikuwa na makosa na imefanyiwa maboresho 20/05/2019)