Injini za ndege kutoka Urusi zilikuwa maarufu pia miaka mingi iliyopita kabla ya taifa hilo kuporomoka na kuvunjika kutoka Umoja wa Kisovyeti. Baada ya miaka mingi sasa tayari ni rasmi utengenezaji wa injini za ndege kutoka kiwanda cha ndani cha taifa hilo umefanikiwa.
Jumanne ya wiki hii ndio kwa mara ya kwanza ndege iliruka nchini humo ikiwa inatumia injini zinazotengenezwa ndani ya nchi hiyo. Ndege hiyo inayokwenda kwa jina la MC-21, imetengenezwa na kampuni inayokwenda kwa jina la Irkut Corporation, injini zikitengenezwa na kampuni ya United Engine Coorporation – asilimia kubwa ya umiliki katika makampuni hayo unamilikiwa na shirika la anga la Urusi la Rostec.
Majaribio ya ndege hiyo yalikuwa ya muda wa saa moja na dakika 25.
Serikali ya Urusi imekuwa imetaka kwa muda mrefu sekta hiyo irudi katika kiwango cha ubora wa juu ili kuweza kushindana na Boeing pamoja na Airbus – mashirika ya utengenezaji ndege ya Marekani na Ulaya.
Inategemewa wateja wa kwanza wa ndege ya MC-21 wataanza kupokea ndege zao kufikia mwisho wa mwaka huu. Hadi sasa kuna oda ndege 175 za MC-21, 50 kati yake zikiwa kutoka shirika la ndege la kiserikali la Urusi, Aeroflot. Ndege hizi zinauwezo wa kubeba abiria 130 hadi 211.
No Comment! Be the first one.