Baada ya uzinduzi rasmi wa Infinix ZERO 6 nchini Tanzania, simu yenye teknolojia ya Artificial intelligence, wengi wamekuwa wakihoji kuhusiana na ufanyaji kazi wa teknolojia hiyo, hivyo basi leo ningependa kuwajuza namna teknolojia ya AI kwenye kamera za Infinix ZERO 6 inavyofanya kazi.
Pamoja na sifa zingine nzuri za infinix ZERO 6, sifa kuu zaidi ya Infinix ZERO 6 ni kamera, Infinix Zero 6 imewekwa nguvu nyingi sana upande wa kamera ambapo kamera za nyuma ni MP 12+MP 24 zenye kupiga picha/picha jongefu na mng’ao wa hali ya juu sana, na kamera ya mbele ni MP 20.
Na katika kuongeza ubora wa kamera ndipo teknolojia ya AI inapofanya kazi sambamba na kamera. Teknolojia ya AI inaiwezesha ZERO 6 kupiga picha zenye muonekano halisi ya mazingira husika mfano kama ni bahari au ua basi utapata picha zenye rangi halisi ya vitu hivyo.
Vilevile, kioo cha mbele kimewekewa ulinzi kwani ni kioo cha Gorilla chenye inchi 6.2. Uwezo wake wa betri ni 3650 mAh pamoja na XCharge kwa ajili ya teknolojia ya kuchaji haraka.
Mbali na kamera, imekuwa ni kama tamaduni kwa Infinix kuzalisha simu zenye muonekano wa kuvutia na safari hii wanatupa asilimia 100% kwani wamehama kabisa kutoka material ya plastiki na chuma chepesi hadi kwenye aluminum.
Infinix imezingatia swala la rangi, imekuja na rangi tatu tofauti Milan Black, Sapphire Cyan na Champagne Gold, simu hii inapatikana nchi nzima .
Sifa Za Infinix ZERO 6 Kwa Ufupi |
Uwezo wa Mtandao: 4G/3G/2G |
Toleo Endeshaji: AndroidTM 8.1 |
Kioo: 6.18 INCH FHD+ |
Prosesa: Qualcomm SDM 636 |
Ukubwa: 156.8*75.9*7.95mm |
ROM + RAM: 64GB + 6GB |
Ujazo Wa Betri: 3650mAh |
Kamera Ya Mbele: 12MP AF+24MP AF Ikiwa Na Uwezo Wa Flash |
Kamera Ya Nyuma: 20MP 4IN1 Ikiwa na Uwezo Wa Flash |