Kupitia ukurasa wao wa Instagram, kampuni ya simu za mkononi Infinix Mobile Tanzania wametoa tamko kwamba baada ya Infinix S5 sasa wanakuja na Infinix S5 Pro ikiwa ni muendelezo wenye maboresho.
Hata hivyo Infinix hawakutoa sifa za simu hio lakini inasemekana itakuja na Kamera inayotokeza kwa juu (Pop up Camera) na meboresho mengine hasa upande wa Kamera na ujazo (storage).
Hii ni moja ya Ishara kwamba Biashara bado zinaendelea japokuwa kuna ugonjwa uliotikisa dunia, COVID19. Ni matumaini ya makampuni mengi janga hili litaweza kupita ndani ya muda mfupi na mambo yakarudi kama kawaida.
Kupitia kurasa zao za mitandao ya kijamii, Infinix wamesisitiza wateja wao kuchukua tahadhari na kujikinga na maambukizi hayo hatari na pia wameweka mazingira salama katika maduka yao yote.