Fununu ambazo si rasmi ila tayari zinasambaa na kwa baadhi ya nchi zisha achiwa huru juu ya kampuni ya simu INFINIX MOBILE kuja na simu Mpya aina ya INFINIX NOTE 12 VIP.
kampuni hii inaleta toleo hili la simu ikiwa ni muendelezo wa Infinix Note 12, simu hii inakuja na maajabu mengi ambayo hayajawahi kufanyika kwenye matoleo ya nyuma kwa upande wa NOTE kutoka Infinix.
BETRI (BATTERY)
Infinix imekua ikisifiwa na inaongoza kwa kutoa matoleo yanayo kaa na chaji zaidi kuliko simu nyingine, hii inatokana na sifa za kila toleo hivyo tetesi zinavuma kua Simu hii Note 12VIP kutoka infinix inakuja na bettry 4500mAh.
Ila hii sio kubwa kinacho shangaza ambacho hata TeknoKona pia tunasubiri kujaribu simu hii kutokana na uvumi huu ni kasi ya kuchaji simu hii inachukua dakika 17 tu.
Kwa Note 12 VIP iliyo zima chaji kabisa kuijaza kufika 100% ndani ya dk17, kwa lugha nyepesi simu hii ni ‘fast charge‘ na ni zaidi ya balaa kwenye soko la simu pamoja inakuja na watts 120w.
PROSESA (PROCESSOR)
Simu hii ya infinix Note 12 VIP inakuja na processor kubwa ya G96 hii kitaalamu inaitwa mediateck Helio G96 ambayo ni MT6781 na ni 12nm ukubwa wa uchakatuaji wa simu hii ni mkubwa kulinganishwa na simu nyingine ambazo zishawahi kutokea huko nyuma…
…na hivyo kuleta namna ya utofauti ndani ya simu hii ambayo inaupa uwezo mkubwa wa ufanisi wa simu, kwa wale wapenzi wa kucheza magemu simu hii ina wafaa sana na wale wapenzi wa movie ina wafaa
Pia zaidi kwa wale watumiaji wa simu kiofisi yaani document zaina tofauti ma file makubwa yote unaweza kufungua kwa wakati mmoja na bila simu yako kuganda ganda (stuck).
REFRESH RATE
Ujio huu wa simu hii unatarajiwa kuwa watofauti kwani simu hii itakuja na kioo chenye uang’avu wa ajabu na zaidi kina kiwango cha kuonyesha upya chenye kasi zaidi yaani refresh rate yake ni 120hz
Hii iko fasta na chap kwenye simu hii, fahamu zaidi juu ya refresh rate na si refresh rate tuu bali kioo chake kina picha halisia yaani Amoled display kinakupa uwezo wakuona vitu kwa ubora (quality) wa juu zaidi tofauti na ukitazama kwenye simu nyingine.
KAMERA (CAMERA)
Infinix Note 12 VIP inakuja na camera ya 108mp, hii ni camera ya juu zaidi hakika itawapa nafasi watumiaji wa simu haswa kwa wale wanao penda picha zaidi.
Haikuwa rahisi kwa kampuni hii japo ilishatoa aina au kameara yenye uwezo wa juu hivi hapo nyuma kwa toleo la Zero X Pro kwa imeongeza cheche na matumizi makubwa ya kamera kwa toleo hili.
Inasemekana simu hii katika kamera itakua na Wide ambayo ni 108 MP, f/1.8, (wide), 1/1.67″, 0.64µm, PDAF, Laser AF pia na Ultra wide yenye 13mm f/2.2 na depth ambayo iko na 2 MP, f/2.4 na uwezo wa video ni 1440p@30fps, 1080p@60fps.
BEI (PRICE)
Hata na baada ya kuwa na vitu vyote hivyo bado simu hii inasemekana ni ya kawaida sana yaani ni kwaajili ya watanzania na waafrika hivyo haitakua na bei kubwa
Jiandae kufurahia ulimwengu wa teknolojia ndani ya simu mpya kutoka infinix itakayo kuja siku chahce zijazo
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako, Niandikie Hapo Chini Katika Uwanja Wa Comment, Hii Umeipokeaje Maana Infinix Kila Siku Wanaboresha Simu Zao?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.