Unapoizungumzia Infinix Hot 10t ni simu janja ambayo ina wiki tu tangu kuzinduliwa kwake na tayari inaweza kupatikana nchini Tanzania kwa urahisi tuu.
Ni nadra sana kwa simu kuzinduliwa kisha kuanza kupatikana nchini Tanzania ndani ya wiki moja tangu kuzinduliwa kwake lakini hilo limewezekana kwa rununu Infinix Hot 10t ambayo kwa haraka haraka tuu ina uwezo mkubwa kwenye kamera lakini pia upande wa betri ipo vizuri.
Sifa za Infinix Hot 10t
Hii ni simu yenye uwezo ingawa si wa juu sana lakini inakidhi kwa kile ambacho soko linataka hususani kuweza kutumia simu janja vizuri kwa ajili ya kucheza gemu bila kukwamakwama. Mbali na hilo utapate kufahamu sifa zake kinagaubaga.
- Ukubwa: inchi 6.82 (720 x 1640px)
- Ubora: IPS LCD sana+umbo mithili ya tone la maji kwenye kamera ya mbele na uso wa nyuma ni plastiki
- Diski uhifadhi: 128GB+uwezo wa kuweka memori ya ziada
- RAM: GB 4
- Kamera Kuu: MP 48, 2 na ya tatu sifa zake hazijajulikana+taa tatu za kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu
- Kamera ya Mbele: MP 8+taa mbili za kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu
- Li-Ion 5000 mAh
- Micro USB 2.0, OTG
- MediaTek Helio G70 SoC
Programu Endeshi
- XOS 7.6, Android 11
- Nyeusi, Kijani, Bluu, rangi ya bahari na Zambarau
Kuhusu kupatikana nchini Tanzania
Infinix Hot 10T ambayo pia inakubali mtandao wa 4G Tigo Tanzania ndio wameamua kuifanya simu hii ipatikane kirahisi kwenye maduka yao nchi nzima. Pia, ina uwezo wa kudumu na chaji kwa muda wa saa 24 huku ikiwa kwenye matumizi ya intaneti. Mbali na hilo wateja watapata GB 78 za intaneti BURE kutumia kwa muda wa mwaka mmoja.
Kuhusu bei yake ni kwamba mpaka tunaingia mtandaoni kuandaa makala hii Tigo Tanzania walikuwa bado hawajaipandisha kwenye tovuti yao lakini kwa bei ya ughaibuni inakaribia $169| zaidi ya Tsh. 390,172.
Vyanzo: Tigo Tanzania, GSMArena
No Comment! Be the first one.