Moja ya programu tumishi ambayo imetokea kupendwa sehemu nyingi duniani katika kipindi cha muda mfupi ni TikTok na katika siku za karibuni kampuni mama imejikuta katika hali ngumu kutokana na kashfa mbalimbali dhidi yao.
Kama ni wakati mgumu basi TikTok inapitia mengi hivi sasa na tayari tumeshasikia kuhusu amri ya kufungwa kutumika huko nchini Marekani lakini pia Instagram kuleta “Reels” na kuonekana kama mpinzani. Kama hiyo haitoshi hivi karibuni imebadika taarifa kuwa katika kipindi cha angalau miezi kumi na mitano (15) TikTok ilikusanya taarifa za watumiaji wake na kuzituma kwenye kampuni mama, ByteDance.
Inaelezwa kuwa katika kipindi hicho TikTok iliwazunguka Google kwa maana ya kwamba watumiaji wa Android hivyo wakawa wanachukuwa taarifa za kitambulisho cha kifaa (Mac address), utambulisho wa akaunti ya mhusika (advertising ID) na kisha kuzipeleka ByteDance kisha kuwapa makampuni yanayotangaza biashara wakatengeneza tangazo kulingana na kile ambacho mhusika anapenda kufanya kwenye TikTok kisha mtumiaji kuendelea kuona tangazo mpaka plae atakapoacha kutumia programu tumishi husika.
Fahamu ya kuwa kwenye vifaa vyetu vya kidijitali kuna kitambulisho ambacho hakibadili, hakifanani na kingine. Kitu hicho kinaitwa Mac address.
Kitendo ambacho inaaminika TikTok walikifanya kwa mujibu wa taarifa iliyotoka hivi karibuni inakiuka kanuni za Google ilizoziweka kwa waundaji wote wa programu tumishi kuhusu ukusanyaji wa taarifa za watu.
Vyanzo: Android Police, Business Insider
2 Comments
Comments are closed.