Nchi ya Korea Kaskazini imeendelea kudhihirisha utata wake hasa katika kukataa aina yeyote ya ushawishi kutoka nchi za magharibi, safari hii nchi hiyo imeanzisha huduma yake ya Manbang ambayo ni kama ile ya Netflix ambayo ilianzishwa nchini Marekani.
Video Ikionesha namna ya kuchagua na cha kuangalia katika Manbang
Manbang pamoja na mambo yote itawaruhusu watumiaji kuweza kuangalia vipindi mbalimbali ambavyo ni maarufu katika mtandao, pamoja na hiyo watumiaji wa huduma hii wanaweza kupata chaneli tano ambazo zinarusha matangazo mubashara ambayo yanaelimisha jamii.
Tofauti na Netflix huduma hii ya Korea Kaskazini inahusisha vipindi na video ambazo zimekaguliwa na kupitishwa na serikali lakini pia hakuna vipindi ama chaneli nyingi ambazo unaweza kuziangalia kama vile ambavyo vipo Netflix.
Hatahivyo inaripotiwa kwamba kutokana ukweli kwamba ni watu wachache ambao wana intaneti majumbani kwao basi ni watu wachache tu ndio wata pata huduma hii ya burudani.
Korea Kaskazini inasifika kuwa na utawala wa kidikteta ambao umekuwa katika migogoro ya kisiasa na nchi nyingi za magharibi hii imepelekea hata tamaduni na teknolojia kutoka magharibi kupata wakati mgumu kupenyeza katika soko la nchi hiyo.