Xiaomi Redmi 9A ni simu janja ambayo hivi karibuni tuu ilitokea kwenye orodha ya rununu ambazo zilifanya vizuri kimauzo mwezi Januari 2021. Je, unafahamu sifa zake?
Xiaomi Corporation ni kampuni ambayo inakuwa kwa kasi sana na yenye makao yake makuu huko Beijing-Uchina ambapo ilianzishwa mwezi Aprili mwaka 2010 na katika kipindi kifupi tuu bidhaa zake zimeweza kupenya maeneo mengi duniani na kuuzika kiasi cha kuwa miongoni mwa kampuni zinazofanya vizuri kimauzo katika miaka ya karibuni.
Xiaomi Corporation ina bidhaa nyingi tuu sokoni na mojawapo kati ya hizo ni Redmi 9A ambayo ilizinduliwa Juni, 30 2020 na kuingia sokoni Julai 7. Ni simu janja iliyonipa shauku ya kutaka kujua ina sifa gani hasa za kuifanya kuwa miongoni mwa zile zilizofanya vizuri kimauzo mwezi Januari 2021? Niseme tuu fuata nami mpaka mwisho wa makala hii. Tuanze na:
Kioo :
- Ukubwa: inchi 6.53 (720×1600 px)
- Ubora: IPS LCD
Memori :
- Diski uhifadhi: GB 32, GB 64 na 128GB+uwezo wa kuweka memori ya ziada mpaka GB 512
- RAM: 2GB, 3GB, GB 4 na GB 6
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 13+taa moja ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu
- Kamera ya Mbele: MP 5
Betri/Chaji :
- Li-Ion 5000 mAh
- USB 2.0, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 10W
Kipuri mama :
- MediaTek Helio G25
Uzito :
- Gramu 196
Programu Endeshi
- MIUI 12, Android 10
Rangi/Bei :
- Kijani, Kahawia na Bluu
- Kwa bei ya chini kabisa kwa maana yenye 2G/32G inaweza kuanzia Tsh. 250,000 kwa Tanzania. Bei inaweza kubadilika kulingana na muuzaji mwenyewe.
Ukizungumzia muonekano, ubora wa betri, memori na bila kusahau bei yake kuwa inayohimilika naamini ndio vitu vilivyochagiza kuweza kufanya vizuri sokoni na kuifanya kampuni husika kuendelea kung’ara kwenye soko la ushindani. Je, una mawazo tufauti? Tuangependa kusikia kutoka kwako.
Vyanzo: GSMArena, Gadgets 360 na mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.