Simu janja za Samsung zimeendelea kuongezeka ambapo takribani wiki mbili zilizopita Galaxy A52s 5G ilizinduliwa ikiwa tayari kwa wale wanaopenda kupata raha ya 5G.
Simu janja ambazo zinatumia 5G zimeendelea kuongezeka ambapo Samsung wameonekana kuendelea kutoa rununu ambazo zinatumia teknolojia hiyo ya kisasa zaidi lakini pia yenye kasi. Samsung Galaxy A52s 5G ina mengi ya kuielezea ambayo yanaifanya simu hiyo ivutie. Sifa zake ni hizi:
Muonekano|Kioo
Hii ni rununu ambayo si pana (unene wake ni 8mm) na wala yenye uzito unaoudhi. Urefu wa kioo chake ni inchi 6.5 (1080*2400px, 120Hz), kioo chake ni cha ung’avu wa hali ya juu (Super AMOLED) na kamera ya mbele imewekwa katikati; inagwa pande mbili za kioo cha mbele mbele iliyowekwa chini ya kioo lakini katika mtindo wa kufanya mbele kuwepo kwa shimo dogo; kamera ya mbele ina MP 32.
Kipuri mama|Memori
Kwenye teknolojia ndani ya simu janja husika Samsung wameamua kuweka Qualcomm Snapdragon 778G 5G huku kwenye kipengele cha memori simu hii ina GB 128/256-diski uhifadhi+uwezo wa kuweka memori ya ziada. RAM ni GB 6 au 8.
Betri|Kamera
Kivutio cha wengi kwenye simu janja mbali na vitu vingine lakini ubora wa kamera, uwezo wa betri huwa vinachochea kwa namna yake kuifanya rununu iuzike kirahisi. Betri ya kwenye simu hii ina 4500mAh, 25W ya teknolojia kuchaji haraka, inatumia USB-C 2.0.
Mengineyo
Simu hii ipo ambayo inatumia kadi mbili za simu na toleo jingine inatumia kadi moja tu ya simu, inalindwa na kioo cha Gorilla 5 upande wa mbele na nyuma ni plastiki, inatumia Android 11, teknolojia ya kutumia alama ya kidole imewekwa chini ya kioo, inapatikana katika rangi Nyeusi, Nyeupe, Zambarau.
Bei yake ni $493|zaidi ya Tsh. 1,133,900 (6/128GB), $513|zaidi ya Tsh. 1,179,900 (8/128GB) na $610|zaidi ya Tsh. 1,403,000 (8/256GB) bei ya ughaibuni na tayari imeshaingia sokoni tangu Septemba Mosi.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
One Comment