Mamlaka ya safari za anga nchini Australia, CASA imefahamisha kuwa mradi wake wa huduma ya usafiri wa kukodi njia ya anga unakaribia kukamilika.
Katika safiri huo wa kukodi kwa njia ya anga yapo makampuni mbalimbali yameshajitokeza kutaka kuwekeza nchini humo na mojapawapo ikiwa Uber ambao tayari walishakaa meza moja na wahusika kujadili suala hilo.
Usafiri huo ni sawa na kukodi helikopta isipokuwa tu wenyewe utakuwa ni wa gharama nafuu zaidi. Mbali na hapo watakuwa wanatumia njia maalum ambazo zitakuwa zinaongozwa na taa za barabarani.