Huduma ya ulipaji matibabu ya Safaricom, M-Tiba imetambuliwa ulimwenguni kama teknolojia inayobadilisha maisha ya wananchi wa Kenya kwa kurahisiha jinsi ya kupata huduma za afya.
Huduma hiyo imeungana na huduma zingine zilizotambuliwa ulimwenguni kama vile Twitter, Spotify na Google ambazo zimebadilisha maisha katika jamii. Lakini M-Tiba ni nini? M-Tiba ni programu tumishi/huduma inayomuwezesha wananchi kulipia huduma za matibabu au kununua madawa hospitalini kwa kupitia M-Pesa.
Tangu kuanzishwa kwa M-Tiba mwaka 2016 imeweza kutumiwa na watu zaidi ya milioni moja huku watoa huduma za afya 700 wanakubali kupokea malipo/muamala uliofanyika kupitia M-Tiba.
Huduma hiyo inayotolewa kwa njia ya programu ilitambuliwa na World Economic Forum (WEF) na M-Akiba ni miongoni mwa kampuni tatu kutoka barani Afrika ambazo zilitambuliwa mwaka huu.