Kampuni ya Huawei ni moja kati ya makampuni makubwa sana duniani katika uzalishaji na uuzaji wa simu. Hivi karibuni kampuni hiyo imezalisha simu zake ambazo zinachata (logo) ya KFC.
Dhumuni kubwa la kuzalisha simu hizi ni kusheherekea maadhimisho ya miaka 30 ya huduma chakula cha haraka huko china.
Huawei sio wa kwanza kutoa simu za muda kulingana na kitu fulani mara nyingi kampuni ya simu ya Samsung na yenyewe imeonekana ikifanya hivyo.
Kwa mfano kampuni ya Samsung ilitoa matoleo kama yale ya Samsung Galaxy S8 toleo la Pirates of the Caribbean , the Samsung Galaxy S7 toleo la Edge Injustice na Samsung Galaxy S6 Edge toleo la Iron Man.
Kwa Huawei hili ndio toleo lake la kwanza ambalo linabeba dhima ya kipekee kama matoleo hayo ya Samsung yalivyo.
KFC ilianzishwa miaka 30 iliyopta huko china, Mpaka sasa KFC ndio mgahawa mkubwa kuliko yote huko China ukiwa umeenea zaidi ya maeneo 5,000.
SIFA ZAKE
Jina la simu ni Huawei Enjoy 7 Plus toleo la KFC
Kioo chake ni Inchi 5.5 720p
Kamera ya MP 12
Prosesa ya Qualcomm Snapdragon 435
RAM GB 3
Ujazo wa uhifadhi GB 32
Kampuni ya Huawei imetengeneza simu hizo 5000 tuu na simu hiyo ikinunuliwa inakuja na vitu kibao ndani ya App ya KFC.
Ni vigumu sana kuona simu hii imetoka nje ya China kwani imezalishwa kwa unit ndogo sana na dhima kubwa ya kutengenezwa ni kusheherekea miaka 30 ya chakula cha haraka. Lakini pengine inaweza ikaonekana katika masoko ya mtandaoni kama vile ebay na Amazon.