Huawei ndio wanaomiliki bidhaa zinazobeba jina la Honor na wameendelea kutoa simu janja kwa mwaka 2018 na kuifanya kuwa ya kiushindani kutokana na bidhaa yenyewe kuwa na mashiko.
Simu janja ambayo imezinduliwa kutoka Honor ni Honor 9i (2018) ambayo inaifanya bidhaa yenye na kampuni mama kuendelea kuwa washindani kwenye soko la simu janja.
Honor 9i ndio simu janja ya kwanza kuwa na kamera nne, kitu ambacho kwa wale ambao kupiga picha au video basi simu hii inakupa nafasi pana zaidi.
Sifa ilizonazo Honor 9i
Simu hii imezinduliwa mwezi Juni 2018 na kwa mujibu wa tovuti mbalimbali imeonekana kupata maoni mazuri. Ina sifa zifuatazo:-
Kioo: Kioo chake kina ukubwa wa inchi 5.84 lakini simu ni ya kitofauti kidogo kwani kioo chake kinaonekana chochote bila ya kuwa na vitu vingine juu yake (full display view).
Prosesa & Betri: Honor 9i ina octa-core HiSilicon Kirin 659 SoC na kile kinachofanya picha zionekane ang’avu (GPU) ni Mali T830-MP2. Betri yake ina 3000 mAh.
Kamera & Programu endeshi: Kamera ya kwanza ya nyuma ina MP 13 na ya pembeni yake ina MP 2 pamoja na LED flash. Kamera za mbele ina MP 16 na kamera zote mbili zinakubali kuchukua picha jongefu katika kiwango cha 1080p.
Diski uhifadhi & RAM: Kwenye diski uhifadhi zipo Honor 9i za aina mbili; kuna zile zenye GB 64 na nyingine zina GB 128 huku zote zikiwa na uwezo wa kukubali uhifadhi wa ziada wa mpaka GB 256. RAM yake ni GB 4.
Kadi za simu & Sifa nyinginezo: Inatumia kadi mbili za simu na zote zikiwa ni zile za kukata (ndogo). Unaweza kutumia alama ya kidole/uso kuweza kufungua simu. Pia ina teknolojia ya 4G LTE, Wi-Fi 802.11ac, Bluetooth, GPS/ A-GPS, na Micro-USB.
One Comment
Comments are closed.