Makampuni nguli kutoka China yaani Huawei, Oppo, Vivo, na Xiaomi ambayo yapo vizuri katika teknolojia za utengenezaji wa simu janja, yameunganisha nguvu katika kuja na mbadala wa soko la apps la #Google PlayStore.
Mbadala huu unahusisha moja kwa moja soko maarufu zaidi duniani yaani Playstore kutoka Google. ukiachana na kuwa mbadala wa Google playstore bado kampuni imeweka wazi kuwa soko hili pia litakua mahususi kwa ajili ya kupunguza kero kwa wandaaji na wasambazaji wa Apps, muziki, video n.k.
Hili linatokea lakini kumbuka simu zingine yaani Oppo, Vivo, na Xiaomi wao bado wana ruhusa ya kutumia Playstore kwa asilimia 100 ukiachana na wenzao wa Huawei ambao mwaka jana walipatwa na kashfa ya kiulinzi na kiusalama.
Huawei walijikita katika kutengeneza OS yake ili waachane na ile maarufu ya Android ambayo ndio maarufu zaidi na ambayo imewaletea vikwazo vingi katika soko la marekani.
Katie Williams, ambae ni mchambuzi katika Sensor Tower, amesema kuwa app za google ambazo zimazuiliwa china kwa mwaka jana zimetengeneza takribani dola za kimarekani bilioni 8.8. duniani kote.
Simu zote yaani Huawei, Oppo, Vivo na Xiaomi zinachangia kwa asilimia 40.1 kwa simu janja zote zinazouzika duniani, hii ikiwa na maana kuwa asilimia iliyobakia pekee ndio inachokuliwa na simu zingine zilizobakia ukichanganya zile za Apple na samsung. Taarifa hizi ni kwa mwongo wa mwisho wa mwaka 2019.
Licha ya makampuni haya yote kuungana lakini bado haijawekwa wazi kuwa kampuni zote hizi zinachangia asilimia ngapi ili kuhakikisha zoezi hili linatimia.
Teknokona tumelipokea vyema jambo hili, kumbuka hii ni njia moja wapo ya kuimarisha huduma na ushindani ukazidi kuongezeka katika masoko ya Apps. Vile vile kumbuka sio vizuri kumtegemea mtu mmoja katika biashara hivyo hii ni hatua nzuri zaidi kwa samsung.