Taarifa zinasema kwamba Kampuni ya Huawei itasitisha kupeleka bidhaa zake katika soko la Marekani kutokana na vikwazo vingi inavyopata katika nchi hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Huawei, Xu Zhijun alisema waziwazi kuwa mambo mengine hayawezi kubadilishwa na wao Huawei na hawataendelea kulazimisha na kutumia nguvu kubwa katika soko ambalo wanaonekana hawahitajiki.
Huawei itaendelea kuzalisha bidhaa bora na kukidhi mahitaji ya wateja wao na kutengeneza na kuaminika zaidi sokoni.
Kampuni ya Huawei kwa muda mrefu imejaribu kupenya katika soko la Marekani lakini serikali ya nchi hiyo mara kwa mara imekuwa ikirudisha nyuma juhudi za kampuni hiyo.
Katika taarifa yake ya maendeleo ya soko la Marekani Huawei imeonyesha hakuna ufanisi wowote wa mafanikio zaidi ya kushuka siku hadi siku na hivyo kuonekana kwa Kampuni hiyo kuondoka rasmi katika soko hilo.
Mwezi Februari mwaka 2018, wakuu sita wa ngazi za juu wa mashirika ya kipelelezi ya Marekani waliwaagiza wananchi wa Marekani kutotumia simu na vifaa kutoka kampuni ya Huawei. Kujua zaidi kuhusiana na taarifa hiyo BOFYA HAPA.