Huawei ni kampuni ya tatu kwa ukubwa katika maswala ya kutengeneza simu duniani. Kwa sasa ndio kampuni kubwa ambayo inaongozwa kuwa mshindani wa simu za Apple na Samsung.
Toleo lake lililopita katika mfululizo wa Honor lilikuwa ni Huawei Honor 8 na kwa sasa ina ripotiwa kwamba kuna toleo linguine la Honor ambalo lipo njiani.
Ukiachana na kesi ambazo ziliwakumba wakuu wa Huawei kuhusu kuvujisha siri za kampuni bado kampuni hilo limejikita katika kuhakikisha kuwa inawapa wateja wake kile ambacho wanakitaka.
Ripoti hizi bado hazijaweka wazi juu ya jina la simu hiyo (lakini injulikana kuwa ni katika muendelezo ule wa Honor) hivyo basi inaweza ikawa ni huawei Honor 9.
FUNUNU JUU YA SIFA
– Prosesa ya octa-core ya 2.4 GHZ yenye CPU ya Kirin 960
– Display ya inchi 5.7 ya kioo cha Quad HD
– RAM ya GB 6
– Ujazo wa uhifadhi wa GB 128
– Betri ya uwezo wa mAh 3900
– Simu itakuwa na uwezo wa laini mbili
– Inasemekana kuwa itakuja na kamera mbili pia
– Uwezo wa kamera ni Mp 12 kwa kamera ya nyuma na kamera ya mbele ikiwa na Mp 8
– Ina uwezo wa 4G LTE na uwezo wa 4.1
– Itakuja katika rangi ya Gold wakati wa kuzinduliwa
Baada ya kusema hayo hatuna budi kuisubiria simu hii tuone kama sifa na jina vitaendana na fununu ambazo zipo mtaani kwa sasa?
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini sehemu ya comment je ni toleo la simu gani ambalo unalisubiria kwa hamu? Niandikie hapo chini sehemu ya comment.
One Comment
Comments are closed.