Huawei wataendelea kutengeneza simu bila huduma za Google kwenye simu zake hadi mwaka 2021, mwezi Mei.
Hii ni baada ya katazo lilolowekwa na serikali kuongozewa muda wake, mwanzoni katazo hilo lilikuwa liishe mwaka huu.
Katazo hilo linagusu makampuni mbalimbali ya nchini Marekani ikiwepo Google.
Kwa sababu za kiusalama makampuni/mashirika ya nchini Marekani hayatakiwi kutumia vifaa vyovyote au huduma zozote kutoka kampuni ya Huawei. Hawatakiwi kuiuzia kampuni hiyo au kununua huduma yeyote kutoka kampuni hiyo.
Tokea katazo la uwezo wa kutumia huduma za Google Apps kwenye simu zake tayari Huawei washaingiza sokoni simu mbali za hadhi ya juu bila uwepo wa Google PlayStore na apps nyingine muhimu za Google. Simu hizo hazikufanya vizuri sokoni – nje ya China. Hizi ni simu za Huawei Mate 30 Pro na Huawei Mate P40 Pro.
Suala hili limewalazimisha Huawei kuja na soko lao la Apps, ila bado suala hili halitatua tatizo kubwa la kukosa apps na huduma nyingine nyingi kutoka makampuni ya Marekani kama vile apps za Facebook, Instagram, Google Maps, YouTube, Twitter na nyingine nyingi.
One Comment
Comments are closed.