HTC hawapo mbali sana kuleta kitu kizuri mbele ya wateja wake duniani kote kwani baada ya uvumi kuenea kuwa watatoa simu janja mpya mwezi Mei sasa wameweka wazi kabisa tarehe ambayo uzindizi utafanyika.
Imekuwa kama desturi ya makampuni mbalimbali kuendelea kutoa simu rununu ambazo zinatoka katika “Familia” moja kama wamavyofanya Apple, Samsung, Xiomi, n.k HTC nao wameona sasa ni wakati sahihi wakutoa HTC U12+.
HTC U12+ itazinduliwa Mei 23 2018 na kama ilivyo kawaida ya makampuni mengi kutoa bidhaa zaidi ya moja katika siku husika, pengine HTC wakazindua pia HTC U12 ingawa hakuna uhakika kuhusiana kuzinduliwa kwa simu hiyo (HTC U12) katika tarehe iliyotangazwa.
Simu janaja, HTC U12+ ni simu inayoelezewa kuwa ni zaidi ya “Sifa zake” kwa sababu ya vile ambavyo simu hiyo imetengenezwa ili kuifanya HTC iwepo katika ramani nzuri ya kimauzo ya bidhaa zake. Sifa za HTC U12+ ni kama ifuatavyo:-
Prosesa: Qualcomm Snapdragon 845 SoC
Kioo: Kioo chake ni cha LCD chenye ubora wa QHD+ na ukubwa wa inchi 5.99 katika uwiano wa 18:9
Kamera: Ina kamera mbili, mbele na nyuma; kamera ya mbele ina MP 8 kila moja za zile za nyuma zina MP 12 kila moja
Programu endeshi: Oreo
RAM/Diski uhifadhi: Ina RAM GB 6, diski uhifadhi wa GB 64/128
Betri: 3420mAh na betri yake haitoki (ni ya ndani kwa ndani)
Bei yake bado haijawekwa wazi hivyo tusubiri mpaka siku itakayozinduliwa na kwa hakika TeknoKona tutawataarifu mengi zaidi kuhusiana na uzinduzi wa HTC U12+.
Vyanzo: GAdgets 360, EveningStandard
One Comment
Comments are closed.