Baada ya miezi kadhaa ya kukata mahusiano na kampuni ya Huawei, brand ya Honor kuja na laptops zinazotumia programu endeshaji ya Windows 10. Hii ni baada ya kukamilika kwa mikataba ya kibiashara na kampuni ya Microsoft.
Vikwazo vya Marekani dhidi ya kampuni ya Huawei vimefanya makampuni mengi ikiwa ni pamoja na Microsoft kukata mahusiano ya kibiashara na kiteknolojia na kampuni ya Huawei.
Huawei ilibidi wauze biashara nzima ya brand yao ya Honor kwenda kwa kampuni mpya inayomilikiwa na wafanyabiashara mbalimbali wa China inayokwenda kwa jina la Shenzhen Zhixin New Information Technology Co. Ltd., kwa kufanya hivyo kumeepusha brand hiyo kujikuta katika vikwazo vya kushindwa kutumia teknolojia za Marekani kutoka Google, Intel, Microsoft na nyingine nyingi katika utengenezaji wa simu na kompyuta.
Kwa sasa Huawei hawana umiliki wowote katika kampuni hiyo, na wafanyakazi na mfumo mzima wa biashara wa simu za Brand ya Honor unamilikiwa na kampuni hiyo mpya.
Kampuni hiyo itakuwa inaleta laptop zinazoenda kwa jina la MagicBook Pro, na kutokana na kuepuka vikwazo hivyo laptop hiyo imeweza kuja na prosesa ya Intel Core i5. Toleo hili jipya la laptop hizi litaanza kupatikana Januari hii.
Sifa za Honor MagicBook Intel
Ukubwa: Inchi 14
Betri: Wh 57.4 – takribani masaa 12 ya utumiaji
CPU: 8th Intel® Core™ i5 Processor
GPU: NVIDIA GeForce MX150,2G VRAM
RAM: GB 8 DDR3
Diski Uhifadhi: GB 256 SSD
Ports: USB-C /USB-A3.0/USB-A2.0/HDMI/3.5 mm headphone jack
Sauti: Quad-speaker, Dolby Atoms Sound System
Keyboard: Yenye mwanga chini ya vibonyezo
Usalama: Teknolojia ya utambuzi wa alama za vidole /fingerprint
Nje ya Microsoft tayari pia kampuni ya Qualcomm imesema itaendelea kushirikiana na simu za Honor ikiamini kampuni hii mpya haina sifa ya kuwa chini ya vikwazo vya Marekani tena kwani haina mahusiano yeyote na kampuni ya Huawei.
niko nauli kama kuna janja yoyote ya kuweza kupakua Movie kutoka kwenye Netflix app na kuweza kuzitoa kwenye divice moja kwenda ingine ?