Kwa miaka kadhaa sasa Infinix wamekuwa wakiendelea kutoa simu janja ambazo ni mwendelezo wa familia ya “Note” ambapo miezi kadhaa ilitoka Infinix Note 10 Pro.
Familia ya Infinix Note imekuwa ikishindana kwa karibu sana na simu janja za Samsung Note lakini kila moja inajitofautisha kwa namna yake na mwisho wa siku sisi wateja ndio tunatoa hukumu ya mwisho kwa maana ipi imenunulika zaidi kuliko nyingine. Leo hii Infinix imetokea kullivutia jicho langu kutokana na sababu mbalimbali. Simu hii ina sifa zifuatazo:-
Kioo :
- Ukubwa: inchi 6.95
- Ubora: IPS LCD (1080*2460px, 90Hz); ung’avu wa hali ya juu sana+ kamera ya mbele ipo katikati (inagawa kioo cha mbele nusu kwa nusu)
Memori :
- Diski uhifadhi: 64GB/128GB/256GB+sehemu ya kuweka memori ya ziada
- RAM: GB 6/8
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 64, 8 na mbili zina MP 2+taa moja ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu. Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 4K na 1080px
- Kamera ya Mbele: MP 16+Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
Betri/Chaji :
- Li-Ion 5000 mAh
- USB-C 2.0, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 33W
Kipuri mama :
- MediaTek Helio G95
Uzito :
- Gramu 209
Programu Endeshi
- XOS 7.6, Android 11
Rangi :
- Zambarau, Nyeusi na Bluu mpauko
Simu hii imeingia tangu mwezi Juni mwaka huu na bei yake inaanzia Tsh. 600,000 kwenye maduka ya Tigo Tanzania. Kumbuka kufuatilia TeknoKona ili uweze kuhabarika halikadhalika kuelimika kuhusu teknolojia.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.