Samsung wameendelea kutoa simu janja ambapo mwezi Machi 2020 ilitoka Galaxy A41 lakini Septemba mwaka huu wakaona inafaa kuzindua toleo linalofuata ambalo kimsingi lina memori kubwa, kamera zenye ubora zaidi pamoja na mambo mengineyo.
Samsung Galaxy A42 5G ilizinduliwa bila ya sifa zake kuwekwa wazi lakini kwa mujibu wa chapisho kutoka kwa walioitengeneza undani wa rununu husika umeweza kufahamika. Sifa za simu janja husika zinaeleza mengi kuhusu bidhaa yenyewe:
Muonekano+Kipuri mama
Kwa mbele una kioo chenye umbo la herufi “U”, kidoti mithili ya tone la maji kwenye eneo la kamera ya mbele, urefu wake ni inchi 6.6 HD+Super AMOLED. Kipuri ni 8 kwa 1-Qualcomm Snapdragon 750G ambapo kasi yake ni 2.2GHz.
Kamera+Betri
Upande wa nyuma ina kamera 4+taa ya kuongeza ung’avu wa picha; MP 48, MP 8 na mbili zina MP 5 kila moja. Kamera ya mbele ambayo kazi yake ni zile picha za kujipiga mwenyewe ina MP 20. Kuhusu betri ina jumla ya 5000mAh, nguvu ya 15W kwa ajili ya teknolojia inayosaidia kujaza chaji kwa haraka.
Memori
SImu janja yenye kipuri mama cha uwezo wa juu unaenda sambamba na RAM hivyo kwenye Samsung Galaxy A42 5G ina toleo 3 za memori; GB 4, GB 6 na GB 8. Upande wa diski uhifadhi ni GB 128 lakini ikiwa na uwezo wa kukubali memori ya ziada mpaka TB 1.
Mengineyo
Inatumia teknolojia ya 5G, rangi zake ni Nyeusi, Nyeupe na Kawawia. Teknolojia ya kutumia alama ya kidole ipo ndani ya kioo, uzito wake ni gramu 190, Bluetooth 5.0, USB Type-C. Kwa toleo lolote ambalo mtu atanunua diski uhifadhi itakuwa ya GB 128 hivyo tofauti itakuwepo kwenye RAM na rangi tu.
Tayari imeshazinduliwa lakini bado haijaingia sokoni mpaka mwezi Novemba huko Ujerumani na gharama yake inakkadiriwa kuwa zaidi ya $430|Tsh. 989,000. Kiujumla hii ni simu janja ya uwezo wa hali ya juu kulingana na sifa zake. Vipi wewe maoni yako?
Vyanzo: Gadgets 260, GSMArena
No Comment! Be the first one.