Ndio kuna App zimekua zikifanya biashara ya kuuza mihadarati (bangi) katika mtandao kwa muda mrefu tuu na Google wameliaona hilo na sasa wamechukua hatua.
Hatua hii ya kuzitoa App hizo imefika baada ya Google yenyewe kubadilisha vigezo na masharti ya PlayStore. Watu wenye App hizo wanalazimika kutoa kipengele cha kusambaza (delivery) ya mihadarati hiyo.
Kama wakishindwa kabisa kusitisha huduma ya usambazaji basi inawaladhimu Google wenyewe kufuta App hiyo katika soko lao.
Google wamefikia uamuzi huu na katu hawajali hata kama matumizi ya mihadarati yameruhusiwa katika sehemu husika, kwa mfano kuna baadhi ya nchi au maeno ambapo matumizi ya mihadarati yameruhusiwa, lakini Google hawajali hilo.
“Haturuhusu App ambazo zinarahisisha uuzaji na ununuzi wa mihadarati au bidhaa za moihadarati” — Google
Hii imetokea baada ya PlayStore kuongeza au kuboresha vitu ambavyo haviruhusiwi katika soko lao. Hivyo basi App zote zinazojihusisha na jambo hili inabidi kutoa kipengele hicho cha kununua mtandaoni.
Wenye App hizo wamepewa mwezi mmoja tuu ili kuendana na tamko hilo, wote ambao watashindwa kufanya hivyo swala ni kwamba App zao zinaweza hata kufungiwa kabisa.