Google imeinunua kampuni ya Raxium kwa kiasi ambacho hakijawekwa wazi katika uma.
Raxium ni kampuni ambayo imejikita na kutengeneza vioo haswa vile vya teknolojia ya LED, ikumbukwe kua kampuni hii bado sio kubwa sana maana ndio kwanza ina miaka mitano.
Lengo la Google kununua kampuni hii ni kuweza kusaidia katika matengenezo wa vifaa vijavyo vya ‘augmented, virtual na mixed reality’.
Ikumbukwe kuwa aina hii ya vifaa ni ile ambayo ina uwezo wa hali ya juu wa kuaminisha kwamba kitu kipo katika mazingira wakati hakipo kwa kutumia msaada wa kioo cha kifaa (mfano – simu).
Fikiria kwa undani kusu jambo hili, Nadhani unakumbuka kuhusiana na Meta? Kama Hukumbuki Ingia HAPA. Meta –mara ya kwanza facebook — na yenyewe imesema mpka kufikia mwaka 2024 itakua imekuja na vifaa vitatu …
… matata vya VR (‘Virtual Reality’). Pengine labda ndio maana Google imefanya ununuzi huo ili kujihakikishia ushindani wa hali ya juu katika soko.
Hapa kinachofanyika ni kwamba timu nzima ya Raxium inajiunga na timu ya Google, na hii itasaidia katika kuhakikisha wanatengeneza vifaa bora zaidi.
Sisi TeknoKona Tutaendelea kuwa karibu na wewe katika kukuletea vifaa vitakavyozalishwa kwa kutumia Timu hii ambayo imeungana na kuwa kitu kimoja.
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako, Niandikie Hapo Chini Katika Eneo La Comment, Je unadhani Google Itaweza Kabiliana Na Soko La Sasa?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.