Kama utaamua kutafuta kitu kupitia tovuti maarufu ya Google bila shaka utaona kuna tofauti wa muonekano wa ukurasa wake katika siku chache zilizopita.
Tofauti hiyo utakayoiona ni mabadiliko yaliyofanywa na wenyewe Google katika kuboresha ukurasa wake. Mabadiliko hayo yanapatikana kwa watumiaji wa simu janja wa mifumo endeshi ya Android na iOS. Kwa watumiaji wa kompyuta hakuna mabadiliko hayo.
Mabadiliko hayo utayaona katika boksi lake la msingi la utafutaji wa vitu mbalimbali ambapo sasa pembeni kumekuwa na mkunjo wa mviringo badala ya muonekano wa awali ambapo kulikuwa na ncha kali bila ya mviringo. Na kisha utaona mabadiliko mengine pale utakapo tafuta kitu na yatakapokuja majibu ya kile ulichotafuta utaona matokeo yote ya utafutaji yapo ndani ya mzunguko wa boksi maalum.