Kwa muda mrefu umekuwepo uvumi kuwa Google wapo mbioni kutoa kitu ambacho kinafanya kazi sawa na AirDrop ya Apple hatimae sasa sio uvumi tena bali ni kweli.
Hapo awali iliaminika kuwa huduma hii ingeitwa FastShare lakini jina limebadilika ingawa misingi ya kazi yake imebaki kuwa illeile na kwa sasa inapatikana kwenye baadhi ya Google Pixel, simu za Samsung na hapo baadae kipengele hicho kitaweza kufanya kazi kwenye rununu zinazotumia Android 6 na kuendelea.
Nearby Share maana yake ni nini?
Hiki ni kipengele kwenye simu za Android kuweza kutuma na kutokea vitu kutoka rununu moja kwenda nyingine. Simu janja mbili zinazotumia Android zinakuwa karibu na mtumiaji ana chagua kile ambacho kukituma kwenda kwenye simu ya pili. Mtu anayepokea anaweza kuudhisha/kusitisha mchakato wa kutokea kitu kutoka kwa anayekituma.
Kipengele hicho kikiwashwa kinampa uwezo wa kuchagua nani wa kumtumia aliyopo kwenye orodha ya majina ya watu aliwahifadhi, waliowaficha lakini hata kuweza kupokea kitu kutoka kwa mtu ambae hujamuhifadhi kwenye rununu.
Simu za Android mbioni kuweza kutumiana vitu kwa njia mbalimbali ikiwemo ile isiyohitaji intaneti kupitia Nearby Share.
Pia, kwenye Nearby Share mtu anaweza akaamua simu gani iwezekuiona au isiyonekane kabisa na inaelezwa kipengele hicho kitaanza kupatikana kwenye Chromebook ndani ya siku za usoni. Vilevile, kwenye maboresho ya hapo baadae kitu hicho kitaweza kufanya kazi kwenye Windows, iOS/macOS.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|