Google watambulisha Google Pixel 3A na 3A XL katika kongamano lao kubwa la Google IO linalohusisha watafiti na waandishi habari muhimu katika sekta ya bidhaa za teknolojia.
Siku chache zilizopita Google wametambulisha Google Pixel 3A na 3A XL katika kongamano lao kubwa la Google IO linalohusisha watafiti na waandishi habari muhimu katika sekta ya bidhaa za teknolojia.
Katika simu ya hizi Google wamefanya mabadiliko machache ukilinganisha na toleo lililopita la Pixel 3, kikubwa ikiwa kwenye eneo la bei na hivyo kuondolewa kwa baadhi ya sifa. Wamezileta katika bei inayoonekana ni nafuu zaidi kwa simu za kisaa za Google Pixels, simu za Pixel 3A zinaanza kupatikana kwa takribani Dola $400 ambapo inamaanisha ni takribani milioni 1 za kitanzania.
Sifa za Google Pixel 3A
Ingawa inapatikana kwa takribani nusu ya bei ya toleo lililopita la Pixel 3, bado simu ya Pixel 3A inakuja na kamera yenye uwezo mkubwa ikibeba sifa kadhaa kutoka toleo lililopita.
Moja ya sifa kubwa kwa mtu utakayenunua simu hizi ni pamoja na uhakika wa kupata masasisho (updates) ya matoleo mapya ya Android kwa wakati bila kuchelewa katika kipindi cha miaka mitatu.
- Inakuja na disk ujazo ya GB 64
- Inakuja na prosesa ya Snapdragon 670
- Diski uhifadhi wa GB 64
- Teknolojia ya eneo la kuchomeka earphone – headphone jack.
- Toleo kubwa la Pixel 3A linakuja na display/kioo cha Full HD OLED cha ukubwa wa inchi 6 wakati ndogo ni ya ukubwa wa inchi 5.6
- Toleo kubwa yaani, Pixel 3A XL linakuja na betri la mAh 3,700 wakati la 3A linakuja na betri la mAh 3,000.
Toleo hili la Pixel halitakuwa na uwezo wa kuzuia maji (water resitance) na uwezo wa kuchaji bila waya (wireless).
Teknolojia ya kuchaji bila umeme ambayo ilikuwepo kwenye toleo lilolopita (Pixel 3) imetolewa, teknolojia ya wireless charging huwa inapatikana kwenye simu zenye sifa ya bei iliyo juu kuliko hii. Na inaonekana Google wameona sio mbaya kuacha na teknolojia ambazo zingeongeza gharama katika utengenezaji wa simu.
Kamera;
Teknolojia katika kamera ya nyuma:
- Megapixel 12.2 (dual-pixel)
- Yenye uwezo mkuwa wa kugundua vitu na kukusaidia kwenye kufocus (Autofocus) pamoja na uwezo wa kupiga picha nzuri ata pale picha inapopigwa wakati wa mitikisiko (electronic image stabilization)
- ƒ/1.8 aperture
- Teknolojia katika urekodi wa video (1080p @ 30fps, 60fps, 120fps; 720p @ 30fps, 60fps, 240fps pamoja na
4K @ 30fps)
Teknolojia katika kamera ya selfi:
- Megapixel 8
- f/2.0 aperture
- Teknolojia katika urekodi wa video (1080p @ 30fps, 720p @ 30fps, 480p @ 30fps)