Kama kuna simu ambayo ilikuwa na fununu nyingi katika miezi ya karibuni rununu Google Pixel 3 na 3 XL zinaongoza lakini baada ya mengi kusemwa sasa simu hizo zimetambulishwa rasmi.
Google imeweka wazi sifa za simu ambazo kwa kweli ziliongelewa sana katika siku za karibuni kuhussina na uwezo wa bidhaa husika, muonekano, kamera, n.k. Sasa hayo yote tuyaache na fahamu sifa rasmi za Google Pixel 3 na 3 XL.
Kipengele |
Pixel 3 |
Pixel 3 XL |
Kioo | Kioo kina urefu wa inchi 5.5 AMOLED, 2160 x 1080 pixels | Kioo kina urefu wa inchi 6.3 AMOLED, 2960 x 1080 pixels |
Muonekamo | Inafanana sana na toleo la 2 XL | Inaendana kama simu za Huawei, OnePlus na Vivo zote za mwaka 2018 |
Kipuri mama | Qualcomm Snapdragon 845 kasi yake ikiwa 4x 2.5GHz na Adreno 630 ubora wa ung’avu | Qualcomm Snapdragon 845 na kasi yake ikiwa 4x 1.6GHz na Adreno 630 ubora wa ung’avu |
Kipengele |
Pixel 3 |
Pixel 3 XL |
Kamera | Kamera moja nyuma na mbili upande wa mbele; ile ya nyuma ina MP 12.2 na za mbele zote mbili zina MP 8 kila moja. | Kamera moja nyuma na mbili upande wa mbele; ile ya nyuma ina MP 12.2 na za mbele zote mbili zina MP 8 kila moja. |
RAM/Diski uhifadhi | 4 GB RAM, 64/128GB memori ya ndani | 4 GB RAM, 64/128GB memori ya ndani |
Betri |
|
|
Kipengele |
Pixel 3 |
Pixel 3 XL |
Bei |
$799|Tsh. 1,837,700 (64GB), $899|Tsh. 2,067,700 (128GB) |
$899|Tsh. 2,067,700 (64GB), $999|Tsh. 2,297,700 (128GB) |
Rangi |
Nyeusi, Nyeupe na Udhurungi |
Nyeusi, Nyeupe na Udhurungi |
Mengineyo |
|
|
Simu ndio hizo ambazo zilikuwa zinaongelewa kwa sana lakini bado hazijaingia sokoni. Mbali na hapo kuna bidhaa nyingine mbili ambazo zilitoka pamoja na Pixel 3 na 3 XL.
Vyanzo: Forbes, The Verge