Mojawapo ya changamoto kubwa kwenye ulimwengu huu wa utandawazi ni ueneaji wa habari za uongo ambapo kutokana na ukuaji wa teknolojia inachukua chini ya sekunde moja kuwafikia watu wengi duniani.
Google ni kampuni kubwa duniani na inawezesha watu kuweza kupata taarifa mbalimbali kuhusu yanayoendelea ulimwenguni. Karibu mwaka mmoja uliopita Google ilifanya jihihada za kuwezesha watu kuweza kutambua habari za uwongo kwa kuwapa watu angalizo kuhusu chanzo cha habari sio cha kuaminika.
Sasa Google wameamua kuboresha zaidi kipengele cha “News” na “Search” kwa kuwafungua watu macho kwa kuwapa elimu ya kuweza kutambua habari za uhakika kwa kuzingatia vigezo hasa kwa mada ambayo inaongelewa sana kupitia vyanzo mbalimbali vya habari.
Katika maboresho ambayo Google imeyafanya mtu anapotafuta habari fulani pia inatoa mapendekezo kuhusu yule aliyeandika habari husika ambapo mtu anaweza kutaka kujua zaidi ili kuweza kujiridhisha kama ni chanzo cha habari cha kuaminika. Pia, kwenye programu tumishi ya News zile habari zinazosomwa sana (top news) zitakuwa zinaonekana za kwanza kabisa kama njia ya kuzipa kipaombele habari ambazo zinasomwa na wengi.
Kwa sasa maboresho hayo yanapatikana kwa watu wa Marekani pekee, inatazamiwa vitu hivyo vitashushwa kwa watumiaji wengi duniani.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mingine
No Comment! Be the first one.