Google Messages-Programu tumishi ya Android inayowezesha mtumiaji kutuma ujumbe mfupi wa maandishi imeboreshwa kwa kuwezesha jumbe kupanda juu kabisa.
Wale ambao tunatumia simu janja za Android tunafahamu vyema programu tumishi ambayo inatuwezesha kutuma ujumbe mfupi wa maandishi kwenda kwa watu mbalimbali ndani ya nchi ulipo; namaanisha Google Messages. Maboresho ambayo yamefanyika inaifanya programu tumishi hudika ifananane na WhatsApp, Telegram.
Kipi kilichoboreshwa?
Kwa mujibu wa Google Messages APK toleo namba 8.1.050 inaonesha mambo mawili mapya kwenye programu tushi husika; mosi ni uwezo wa kupandisha mazungumzo ya watu kuoka chini hadi juu kabisa. Pili, uwezo wa kuweka alama ya nyota kama ishara ya kuupa kipaombele kile ambacho amekijibu ama ulivyomjibu mlivyokuwa mkiwasiliana kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi.
Vipengele hivyo vipya ni sawa kabisa na vile ambavyo mtu anaweza kufanya kwenye Telegram, WhatsApp na nyinginezo. Faida ya kubadilisha mpangilio ni urahisi wa kufuatilia mazungumzo kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno ambapo mtu anataka asiupoteze/uwe unaonekana kiurahisi.
Tungependa kupata maoni yako kutoka kwako msomaji wetu unayetufuatilia kila siku, una lipi la kusema kuhusiana na habari hii?
Vyanzo: Gadgets 360, GSMArena
No Comment! Be the first one.