Google ina huduma nyingi sana, huduma za Duo na Meet ni huduma nzuri kutoka kwao za kuhakikisha kuwa watumiaji wanawasiliana kwa kupitia njia ya video.
Inamaana kwa sasa hudumahii itakua katika mfumo wa mmoj atuu, kitakauchofanyika ni kwamba mgumo wote wa Google Duo utaenda katika Google Meet.
Ndio! Kama ukitaka huduma ya Duo utaipata katika Meet, Hii ni hatua nzuri sana maana watumiaji wa huduma za Google hawahitaji huduma nyingi zenye kazi zinazofanana kutoka katika mtandao huo.
Hii pia imekua ni msaada kwa baadhi ya watumiaji wa huduma hizi, kuna wale waliokua wanasumbuliwa kuchagua kuhusiana na huduma ipi ya kutumia.
Kama zote zitakua zinapatikanaa katika eneo moja adha hiyo haitokuwepo tena. Huduma hizi zinatumika kwa kuunganisha barua pepe na namba za simu za mtumiaji.
Ni wazi kuwa Google Meet imejipatia jina kubwa sana tangia kuzinduliwa kwake na inaweza kuwa ni moja kati ya mshindani mkubwa sana.
App kama WhatsApp inabidi zijiangalie sana maana Google Meet ina uwezo mkubwa sana wa kupata wafuasi wengi sana.
Fikiri ikijiunganisha na huduma zake zingine tuu, itakua na uwezo mkubwa wa kujiongezea watumiaji/wateja.
Wataalam wamesema kuwa Google bado wana kazi kubwa sana ya kufanya katika kuhakikisha kuwa kampuni inaboresha huduma yake hii.
Maboresho hayo ndio yatasababisha huduma hiyo ya Google Meet izidi kuwa kubwa na kuwa mshindani mzuri kwa huduma zingine za simu za Video na sauti kama vile WhatsApp.
Ningependa kusikia kutoka kwako, hili umeliokea vipi kutoka Google, Je unadhani itakua ni mshindnai bora au mambo badoo?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.