Google Map ni kitu ambacho katika dunia ya leo ni msaada katika mambo kadha wa kadha kiasi kwamba imewezesha watu kuwa kujiamini zaidi wakati wanapokuwa kweny mizunguko yao.
Hadi sasa dunia yote inapambana na janga la virusi vya Corona ambalo limegharimu maisha ya mamilioni ya watu. Makampuni mbalimbali yameendelea kuchukua hatua madhubuti katika kukabiliana na tatizo hilo.
Wengi wetu ambao tunatumia vifaa vya kidjiti vyama hasa kwa kuiangazia “Google Map” tunafahamu jinsi ambavyo ni msaada mkubwa katika kumuwezesha mtu kufika mahali anapokwenda bila ya hata kusimama na kuuliza wapita njia; sitaki kwenda mbali zaidi na kuzungumzi Uber, Taxify na nyinginezo jinsi ambavyo kitu kilivyo muhimu kwao.
Sasa katika hali ya kuvutia na kipekee kabisa kuhusiana na mapambano dhidi ya VIrusi vya Corona GOogle Map imefanyiwa marekebisho kidogo na sasa ukifungua/ukitembelea hukoi utakutana na maneno “Search for COVID-19 vaccines” kwenye kisanduku cha kutafuta kitu ndani ya Google Map. Kwa tafsiri isiyo rasmi maneno hayo ni “Tafuta chanjo ya virusi vya Corona“.
Hii imekuwa ni muendelezo tuu kwani kama Google pia wameweka mazingira mazuri tuu ya watu kuweza kupata taarifa, takwimu kuhusiana virusi vya Corona kulingana na nchi/mahali ambapo mtu yupo. Je, huna taarifa? Basi BOFYA HAPA kuweza kufahamu zaidi.
TeknoKona tumeendelea kukuhabarisha kwa siku nyingine tena, unaizungumziaje habari hii? Na je, una swali lolote? Basi usisite kutuandikia nasi tutakujibu.
Vyanzo: 9to5Google, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.