“Sikusikii niko kwenye makelele, tuma meseji” hii tumeshakutana nayo sana sio? Lakini kwa kupitia huduma ambayo inategemewa kuletwa na Android, Clear Calling pengine inaweza ikapunguza adha hii.
Google bado inataka kuboresha zaidi huduma zinazopatikana katika prgramu yake endeshi maarufu ya Android hasa katika toleo la Android 13, hii ikiwemo na kuleta vipengele vingi vizuri kwa watumiaji wake.
Toleo la Android 13 la beta (toleo la majaribio) tayari linakuja na kipengele hiki cha clear calling na lengo lake kubwa ni kupunguza sauti zinazokuzunguka wakati ukiwa unaongea na simu.
https://twitter.com/MishaalRahman/status/1567961700682575874
Hapa dhamira ni kuboresha mawasiliano baina ya pande mbili zinazowasiliana, lakini ukifikiria kwa undani kabisa utakuja kugundua kipengele hicho sio kipya sana.
Kama unakumbuka vizuri ni kwamba spika za masikio nyingi ambazo hazina nyaya zina teknolojia ijulikanayo kama ‘Noise cancellation” na hapa lengo lake kuu ni kuzuia kelele….
… katika mazingira yanayokuzunguka zisiweze kupenya katika masikio na kukuharibia usikivu wa kile unachokisikiliza kupitia spika hizo.
Ni wazi simu hizi kuna teknolojia nyingi sana ambazo kwa namna moja au nyingine zinarahisisha sana maisha kwa watu.
Kibaya ni kwamba kama utakua unapiga simu kwa kutumia huduma ya Wi-Fi basi kipengele hichi hakitakuunga mkono, hii ni kwenye simu za kawaida tuu (Mobile networks).
Kwa kuanzia tuu wataanza kwenye simu janja zinazotumia Android 13, kwa matoleo ya chini bado hakuna uhakika kama yatapata huduma hii lakini hili sio la kubeza, teknolojia haijaacha kutushangaza.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, je unawapa sifa kaisi gani Google kwa kufikiria hili?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.