Huduma mbalimbali za Google zimeripotiwa kufikia tamati baada ya muda fulani na safari hii Google Hangouts ipo kwenye mlolongo wa kutotumika tena.
Takribani programu tumishi mbili zinazomilikiwa na Google zimebainishwa kuacha kutumia kila moja katika kipindi/mwaka tofauti na hapa nazungumzia Google Plus ambayo itafungwa mwaka 2019 huku Google Hangouts ikifikia tamati mwaka 2020.
Google Hangouts ilianza kutumika mwaka 2013 ambayo kimsingi inatoa huduma ya mawasiliano (kwa maandishi/picha jongefu) kwenye Gmail lakini pia hata jumbe za kawaida kwa maana ya kwamba unaweza kutuma/kupokea ujumbe mfupi wa maneno kutoka kwa mtu anayetumia mtandao wa simu.
Google Hangouts inafikia ukingoni lakini bado tukiwa na programu kama Google Allo na Duo ambazo kimsingi zinavutia na kuwa na vikorombwezo kadha wa kadha.
Vyanzo: GSMArena, 9to5Google, The Verge,