Ikiwa huna mazoea ya kufuatilia kopo la uchafu kwenye Google Drive basi hakikisha unafanya kama tabia kufuatilia kuanzia sasa. Google imetangaza kuwa itafuta faili zote zilizowekwa kwenye kapu la takataka baada ya siku 30.
Hapo awali, Trash folder zilihifadhiwa milele isipokuwa ukienda kwenye kapu la uchafu na ukaifuta kabisa. Hii iliruhusu watumiaji kupata faili kwa urahisi pale anapolihitaji.
Sera hii itaanza kutumika kuanzia Oktoba 13 na mara tu itakapoanza kutumika kutakuwepo taarifa fupi kwenye Google Drive, Hati za Google na Fomu za Google kueleza kuhusu mabadiliko hayo kuanzia Septemba 29. Mabadiliko ya sera yataanza kutekelezwa bila kujali anakubali/kukataa mabadiliko hayo.
Tufahamu ya kuwa kuweka vitu kwenye kapu la takaktaka ndani ya Google Drive kisha kuvifuta kabisa si kwamba vinatoweka kabisa la hasha! Waangalizi wanao uwezo wa kuvirudisha vitu vilivyofutwa ndani ya siku 25 kwa wale watumiaji hai.
Sera za utunzaji zilizowekwa na wasimamizi katika Google Vault haziathiriwi na mabadiliko haya, isipokuwa yatakapopitwa na wakati kwani sasa hayatumiki.
Mabadiliko haya huathiri vitu ambavyo vimetupwa kutoka kwa kifaa chochote na jukwaa lolote maadamu viko kwenye akaunti sawa ya Google. Je, unadhani mabadiliko haya yatamuathiri mtumiaji kwa kiasi gani?
Vyanzo: The Verge, Times of India
No Comment! Be the first one.